Thursday, May 16, 2013
HUDUMA ENDELEVU YA MAJI
Huduma Endelevu ya Maji!
Tarehe 14 Mai 2013 Ubalozi wa Uholanzi kwa
kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Uholanzi SNV liliandaa kongamano kwa
wadau katika sekta ya maji.
Lengo kuu la mkutano huu ulikusudia kujadili kwa
kina umuhimu na upana wa dhana ya uendelevu wa huduma ya maji vijijini. Miradi mingi inapojengwa na kukamilika
inafanya kazi kwa muda mfupi na hivyo haitoi huduma endelevu. Mkutano huu pia ulitoa fursa ya kubadilishana
uzoefu juu ya umuhimu wa suala la uwajibikaji wa kila mdau katika suala zima la
kuboresha upatikanaji endelevu wa huduma ya maji.
Waziri wa Maji Mheshimiwa Profesa Jumanne
Maghembe alifungua Mkutano huu ambao ulihudhuliwa na washiriki kutoka wadau wa
sekta ya maji nchini wakiwemo wabunge, wawakilishi kutoka serikali za mitaa,
mikoa na mashirika ya kimataifa na
kutoka wizara ya maji na Tamisemi.
Katika kufungua Mkutano, Waziri wa Maji
Mheshimiwa Profesa Jumanne Maghembe alisisitiza kwamba ili kujiandaa kwa huduma
endelevu ya maji inahitajika ushiriki wa wadauna wahusika katika
sekta ya maji zikiwemo wilaya,
kata, na vijiji, mashirika yasiyo ya kiserikali na sekta binafsi. Wadau hawa
wanatakiwa kushirikishwa kuanzia katika upangaji wa mipango, utekelezaji, na
ufuatiliaji wa ujenzi wa miundo mbinu na huduma ya maji. Inafahamika kwamba
ushirikishaji wa wadau wote ina changamoto zake kwani inahitaji muda na
rasilimali, lakini mafanikio yake yana manufaa makubwa zaidi.
Utaratibu huu wa kushirikisha wadau wote huleta
mshikamano na uhusiano na uwajibikaji unaohitajika sana kupatikana huduma
endelevu ya maji.
Waziri wa Maji pia alisisitiza umuhimu wa
kuzingatia si masuala ya kiufundi tu wakati wa ujenzi wa miradi mipya ya maji
au ukarabati wa miradi ya zamani:
” Tunahitaji kuwajengea uwezo wananchi amabo
tunawapatia huduma ya maji ili waweze kutimiza wajibu wao katika kuifanya
miradi hiyo iwe endelevu. Tunapoaandaa
miradi lazima tufikirie wale ambao watalipia huduma na uwezo wao wa kulipia”.
Wakati wa majadiliano, washiriki
walisisitiza umuhimu wa namna wadau wanavyotakiwa kushirikiana na kuwajibika
katika kupatikana kwa huduma endelevu ya maji.
Wadau pia waliweza kutambua wajibu wao na nafazi zao na za wadau wengine
katika kuhakikisha kuna ufanisi na hakuna ubaguzi katika utoaji huduma. Pia
waliweza kubaini wanawajibika kwa nani wakati wa kutekeleza majukumu yao. Diwani mmoja aliyeshiriki alisema:
” Vyombo vya watumiaji maji vinakosa
uelewa, kwa mfano kutokana na kukosekana uelewa utashi wa kumilki miradi ya
maji unakosekana. Vyombo vya watumiaji
maji vinatakiwa si kuanzishwa na kusajiliwa tu bali pia kujengewa uwezo. Na vyombo hivi vya watumiaji maji vikisimamiwa
vinaweza kufanya kazi kwa ufanisi’’.
Wakati wa kuhitimisha mkutano huu
maswali na mambo mengi yalijitokeza ambayo yalihitaji kupatiwa majibu wakati wa
uandaaji wa mpango au utaratibu utakaoweza kuimarisha suala la uendelevu wa
uwekezaji katika utoaji huduma ya maji vijijini yakiwemo:
·
Ni
jinsi gani ya kuhakikisha uandaaji wa mipango unazingatia
uwezo wa washiriki wote ili kuweza kuwa na uendelevu wa huduma ya maji na namna
ya kujenga uwezo na kufafanua wajibu na kazi za kila mdau na kuwajengea uwezo
ili waweze kutekeleza majukumu yao na upatikanaji wa rasilimali kwa ajili ya uendeshaji?
·
Ni
jinsi gani tunahakikisha jamii haipatiwi majukumu ambayo haiwezi kuyatekeleza,
tunapotoa majukumu kwa jamii na jamii
haijawa tayari kuyapokea au ni majukumu mazito Je si kuwatupia mzigo jamii?
Kama Mheshimiwa Waziri alivyosema: Ni vipi mkulima wa kawaida anaweza akawa
mhasibu wa mradi mkubwa wa maji awajibikwe kwa fedha nyingi kwa mwezi kiasi
ambacho anaweza kuzipata kwa miaka mingi?
·
Ni
namna gani tunaweza kuhakikisha kuwepo kwa uwajibikaji kati ya jamii na
serikali za mitaa au halmashauri, na pia ni namna gani maswali yaliulizwa yatazingatiwa katika kuandaa mipango na
mikakati (WSDP-II, Big Result Now)?
Mkutano ulifungwa na Naibu Waziri
wa Tamisemi Mheshimiwa Aggrey Mwanry ambaye alisisitiza pamoja na mambo mengine
kwamba, awamu ya pili ya prorammu ya maji (WSDP) izingatie suala la uendelevu
wa huduma ya maji kwani awamu ya kwanza imetupa kujifunza na uzoefu lakini
mkutano umeongeza uelewa katika suala zima la uendelevu wa huduma ya maji.
Naibu Waziri alisisitiza umuhimu wa
kuhakikisha kwamba wataalmu wa halmashauri wanawajibika katika kutekeleza
majukumu yao: Kama huduma ya maji haipatikani kama inavyopaswa, madiwani na
wabunge wawajibishwe na wananchi.
Katika kuhitimisha na kufunga
mkutano, Mheshimiwa Naibu Waziri aliyeshirika muda mwingi wa majadiliano na
kutoa michango iliyoibua majadiliano alikiri kwamba majidiliano yalikuwa
mazuri.
Tuesday, May 14, 2013
REDD'S MISS UBUNGO 2013 KUPATIKANA IJUMAA MEI 17
Baadhi ya washiriki wa Shindano la Redd's Miss Ubungo 2013 wakiwa katika
picha ya pamoja wakati wa mazoezi yao jana. Warembo hao wanataraji
kupanda jukwaani Ijumaa ya Mei 17, mwaka huu katika Ukumbi wa Meeda
uliopo Sinza jijini Dar es Salaam na kusindikizwa na kundi zima la FM
Academia wazee wa Ngwasuma.
picha ya pamoja wakati wa mazoezi yao jana. Warembo hao wanataraji
kupanda jukwaani Ijumaa ya Mei 17, mwaka huu katika Ukumbi wa Meeda
uliopo Sinza jijini Dar es Salaam na kusindikizwa na kundi zima la FM
Academia wazee wa Ngwasuma.
Monday, May 13, 2013
RAIS KIKWETE AZINDUA JENGO LA SAYANSI KATIKA KITUO CHA TAASISI YA KIMATAIFA YA KILIMO CHA TROPIKI LEO (PICHA ZAIDI)
RAIS KIKWETE AZINDUA JENGO LA SAYANSI KATIKA KITUO CHA TAASISI YA KIMATAIFA YA KILIMO CHA TROPIKI LEO
![]() |
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wakati wa uzinduzi wa jengo la
sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki
(IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.
|
USAJILI WA TUZO ZA MUZIKI ZA RFI WAANZA, WANAMUZIKI TANZANIA CHANGAMKIENI FURSA HII
Kwa usajili wa tuzo za muziki za rfi ambazo hufanyika kila mwaka na kuwashirikisha wanamuziki mbalimbali katika bara la Afrika bonyeza hapo chini rfi music award registration
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA MCHUNGAJI DKT. MATHEW BYAMUNGU NA MKEWE IKULU DAR LEO
Subscribe to:
Posts (Atom)



















