Thursday, May 16, 2013

CEO ROUND TABLE WAKUTANA NA KINANA

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahaman Kinana akitoa mada kwenye mkutano wa CEO Round table.


HUDUMA ENDELEVU YA MAJI



                                                        
Huduma Endelevu ya Maji!

Tarehe 14 Mai 2013 Ubalozi wa Uholanzi kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Uholanzi SNV liliandaa kongamano kwa wadau katika sekta ya maji.

Lengo kuu la mkutano huu ulikusudia kujadili kwa kina umuhimu na upana wa dhana ya uendelevu wa huduma ya maji vijijini.  Miradi mingi inapojengwa na kukamilika inafanya kazi kwa muda mfupi na hivyo haitoi huduma endelevu.  Mkutano huu pia ulitoa fursa ya kubadilishana uzoefu juu ya umuhimu wa suala la uwajibikaji wa kila mdau katika suala zima la kuboresha upatikanaji endelevu wa huduma ya maji.

Waziri wa Maji Mheshimiwa Profesa Jumanne Maghembe alifungua Mkutano huu ambao ulihudhuliwa na washiriki kutoka wadau wa sekta ya maji nchini wakiwemo wabunge, wawakilishi kutoka serikali za mitaa, mikoa na  mashirika ya kimataifa na kutoka wizara ya maji na Tamisemi.

Katika kufungua Mkutano, Waziri wa Maji Mheshimiwa Profesa Jumanne Maghembe alisisitiza kwamba ili kujiandaa kwa huduma endelevu ya maji inahitajika ushiriki wa wadauna wahusika  katika  sekta  ya maji zikiwemo wilaya, kata, na vijiji, mashirika yasiyo ya kiserikali na sekta binafsi. Wadau hawa wanatakiwa kushirikishwa kuanzia katika upangaji wa mipango, utekelezaji, na ufuatiliaji wa ujenzi wa miundo mbinu na huduma ya maji. Inafahamika kwamba ushirikishaji wa wadau wote ina changamoto zake kwani inahitaji muda na rasilimali, lakini mafanikio yake yana manufaa makubwa zaidi.
Utaratibu huu wa kushirikisha wadau wote huleta mshikamano na uhusiano na uwajibikaji unaohitajika sana kupatikana huduma endelevu ya maji.

Waziri wa Maji pia alisisitiza umuhimu wa kuzingatia si masuala ya kiufundi tu wakati wa ujenzi wa miradi mipya ya maji au ukarabati wa miradi ya zamani:

” Tunahitaji kuwajengea uwezo wananchi amabo tunawapatia huduma ya maji ili waweze kutimiza wajibu wao katika kuifanya miradi hiyo iwe endelevu.  Tunapoaandaa miradi lazima tufikirie wale ambao watalipia huduma na uwezo wao wa kulipia”.

Wakati wa majadiliano, washiriki walisisitiza umuhimu wa namna wadau wanavyotakiwa kushirikiana na kuwajibika katika kupatikana kwa huduma endelevu ya maji.  Wadau pia waliweza kutambua wajibu wao na nafazi zao na za wadau wengine katika kuhakikisha kuna ufanisi na hakuna ubaguzi katika utoaji huduma. Pia waliweza kubaini wanawajibika kwa nani wakati wa kutekeleza majukumu yao.  Diwani mmoja aliyeshiriki alisema:

” Vyombo vya watumiaji maji vinakosa uelewa, kwa mfano kutokana na kukosekana uelewa utashi wa kumilki miradi ya maji unakosekana.  Vyombo vya watumiaji maji vinatakiwa si kuanzishwa na kusajiliwa tu bali pia kujengewa uwezo.  Na vyombo hivi vya watumiaji maji vikisimamiwa vinaweza kufanya kazi kwa ufanisi’’.

Wakati wa kuhitimisha mkutano huu maswali na mambo mengi yalijitokeza ambayo yalihitaji kupatiwa majibu wakati wa uandaaji wa mpango au utaratibu utakaoweza kuimarisha suala la uendelevu wa uwekezaji katika utoaji huduma ya maji vijijini yakiwemo:

·         Ni jinsi gani ya kuhakikisha uandaaji wa mipango unazingatia uwezo wa washiriki wote ili kuweza kuwa na uendelevu wa huduma ya maji na namna ya kujenga uwezo na kufafanua wajibu na kazi za kila mdau na kuwajengea uwezo ili waweze kutekeleza majukumu yao na upatikanaji wa rasilimali kwa ajili ya uendeshaji?
·         Ni jinsi gani tunahakikisha jamii haipatiwi majukumu ambayo haiwezi kuyatekeleza, tunapotoa majukumu kwa  jamii na jamii haijawa tayari kuyapokea au ni majukumu mazito Je si kuwatupia mzigo jamii? Kama Mheshimiwa Waziri alivyosema: Ni vipi mkulima wa kawaida anaweza akawa mhasibu wa mradi mkubwa wa maji awajibikwe kwa fedha nyingi kwa mwezi kiasi ambacho anaweza kuzipata kwa miaka mingi?
·         Ni namna gani tunaweza kuhakikisha kuwepo kwa uwajibikaji kati ya jamii na serikali za mitaa au halmashauri, na pia ni namna gani maswali yaliulizwa  yatazingatiwa katika kuandaa mipango na mikakati (WSDP-II, Big Result Now)?

Mkutano ulifungwa na Naibu Waziri wa Tamisemi Mheshimiwa Aggrey Mwanry ambaye alisisitiza pamoja na mambo mengine kwamba, awamu ya pili ya prorammu ya maji (WSDP) izingatie suala la uendelevu wa huduma ya maji kwani awamu ya kwanza imetupa kujifunza na uzoefu lakini mkutano umeongeza uelewa katika suala zima la uendelevu wa huduma ya maji.

Naibu Waziri alisisitiza umuhimu wa kuhakikisha kwamba wataalmu wa halmashauri wanawajibika katika kutekeleza majukumu yao: Kama huduma ya maji haipatikani kama inavyopaswa, madiwani na wabunge wawajibishwe na wananchi.

Katika kuhitimisha na kufunga mkutano, Mheshimiwa Naibu Waziri aliyeshirika muda mwingi wa majadiliano na kutoa michango iliyoibua majadiliano alikiri kwamba majidiliano yalikuwa mazuri. 




Tuesday, May 14, 2013

REDD'S MISS UBUNGO 2013 KUPATIKANA IJUMAA MEI 17


Baadhi ya washiriki wa Shindano la Redd's Miss Ubungo 2013 wakiwa katika
picha ya pamoja wakati wa mazoezi yao  jana. Warembo hao wanataraji
kupanda jukwaani Ijumaa ya Mei 17, mwaka huu katika Ukumbi wa Meeda
uliopo Sinza jijini Dar es Salaam na kusindikizwa na kundi zima la FM
Academia wazee wa Ngwasuma.

Monday, May 13, 2013

RAIS KIKWETE AZINDUA JENGO LA SAYANSI KATIKA KITUO CHA TAASISI YA KIMATAIFA YA KILIMO CHA TROPIKI LEO (PICHA ZAIDI)

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais mstaafu  wa Nigeria na Balozi wa heshima wa  IITA Chief Olesegun Obasanjo na Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Benjamin William Mkapa wakizindua rasmi  jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.



 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais mstaafu  wa Nigeria na Balozi wa heshima wa  IITA Chief Olesegun Obasanjo na Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Benjamin William Mkapa katika picha ya pamoja na wadau wa maendeleo bnaada ya kuzindua rasmi  jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais mstaafu  wa Nigeria na Balozi wa heshima wa  IITA Chief Olesegun Obasanjo wakisiliza maelezo ya tafiti mbalimbali za mihogo baada ya kuzindua rasmi  jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na akiangalia katika darubini vimelea vya magonjwa ya mihogo vilivyo katika sehemu ya utafiti baada ya kuzindua rasmi  rasmi  jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.

Rais Mstaafu Mzee Benjamin William Mkapa akiwa na  Balozi wa Marekani nchini Mhe Alfonso E. Lenhardt  pamoja na  Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Mhe. Tonia Kandiero  wakati wa uzinduzi  rasmi  rasmi  jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.

PICHA NA IKULU

RAIS KIKWETE AZINDUA JENGO LA SAYANSI KATIKA KITUO CHA TAASISI YA KIMATAIFA YA KILIMO CHA TROPIKI LEO


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais mstaafu  wa Nigeria na Balozi wa heshima wa  IITA Chief Olesegun Obasanjo na Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Benjamin William Mkapa
wakionja mikate iliyotengenezwa kwa unga wa muhogo wakati wa uzinduzi wa jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais mstaafu  wa Nigeria na Balozi wa heshima wa IITA Chief Olesegun Obasanjo na Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Benjamin William Mkapa wakisikiliza maelezo ya kitaalamu juu ya utafiti wa maradhi ya migomba toka kwa Profesa Rony Swennen  wakati wa uzinduzi wa jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wakati wa uzinduzi wa jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.


Rais mstaafu  wa Nigeria na Balozi wa heshima wa  IITA Chifu Olesegun Obasanjo na Rais Mstaafu wa akihutubia wakati wa  uzinduzi wa jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.

USAJILI WA TUZO ZA MUZIKI ZA RFI WAANZA, WANAMUZIKI TANZANIA CHANGAMKIENI FURSA HII




Kwa usajili wa tuzo za muziki za rfi ambazo hufanyika kila mwaka na kuwashirikisha wanamuziki mbalimbali katika bara la Afrika bonyeza hapo chini rfi music award registration

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA MCHUNGAJI DKT. MATHEW BYAMUNGU NA MKEWE IKULU DAR LEO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mchungaji Dkt. Mathew Byamungu, wakati akimkaribisha Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Mei 13, 2013 alipofika kwa mazungumzo akiwa ameongozana na mkewe, Je-Ynung. Picha na OMR


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mchungaji Dkt. Mathew Byamungu, wakati akimkaribisha Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Mei 13, 2013 alipofika kwa mazungumzo akiwa ameongozana na mkewe, Je-Ynung. Picha na OMR